KTN VIDEO: Buriani Sumbeiyo
Amani sio suala la kulazimishwa bali ni suala ambalo linastahili kutoka ndani ya mioyo ya wakenya, hayo ni matamshi ya Rais mstaafu Daniel Arap moi wakati wa mazishi ya Elijah Sumbeiywo ambaye alikuwa kamanda wa kikosi cha msafara wa rais, katika utawala wake. Rais mstaafu amesema kwamba ile sheria ya utengamano na uwiano sio njia mwafaka ya kuleta amani miongoni mwa wakenya. Wakati wa mazishi hayo wanasiasa waliweka kando tofauti zao za kisiasa na kumpa marehemu heshima yake ya mwisho
